WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO MBINGA WAKABISHIWA VITAMBULISHO



WAFANYABIASHARA  NDOGONDOGO MBINGA WAKABISHIWA VITAMBULISHO

Jumla ya wafanyabishara  ndogondogo 70 kutoka katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga wamekabidhiwa vitambulisho  na Katibu Tawala Wilaya ya Mbinga Bi. Pendo Ndumbaro tarehe 24 Februari 2025.

Moja ya faida ya vitambulisho hivyo ni kuwawezesha  wafanyabiashara hao kutambulika katika mamlaka  mbalimbali hususan  Mamlaka ya mapato Tanzania pamoja  taasisi za kifedha.

Aidha ni fursa mojawapo kwa Halmashauri  katika kujua idadi ya wafanyabiashara  ndogondogo  katika maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga katika kuendeleza / kuboresha miundombinu rafiki ya kibiashara.

Post a Comment

0 Comments